Ndege zote zinazobeba miraa kwenda nchini Somalia zitahitajika kutua kwenye uwanja wa kimataifa wa Aden Abdulle mjini Mogadishu, inasema serikali nchini humo.
Naibu waziri wa biashara na viwanda Mohamed Dirie Khalif, aliyasema hayo wakati akikagua bhari lililopo kwenye uwanja huo ambapo kwanza miraa itahifadhiwa ikisubiri kusafirisha maeneo mbalimbali.
Alisema tarkriban tani 14 za miraa zinatarajiwa kwenye uwanja huo kila siku.
Aidha amedokeza kuwa ndege za miraa kwenda mji wa
Jowhar eneo la Middle Shabelle zimesimamishwa baada ya makubaliano na wadau kwenye sekta hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |