Serikali ya Kenya itaipa hoteli ya Mombasa Beach shilingi milioni 150 ili kuisaidia kuboresha huduma na kuongeza vyumba vya kulala.
Hoteli hiyo inamilikiwa na halmashauri ya utalii nchini humo na ina vyumba 150.
Maneja mkuu wa hoteli hiyo Victor Shitakha, tayari wametoa tangazo la kutafuta mkandarasi atakayefanya ukarabati.
Hoteli hiyo ilipata umaarufu baada ya aliyekuwa rais wa DR cOngo wakati huo ikiitwa Zaire Mobutu Sese Seko, kulala humo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |