Uandikishaji wa wapiga kura katika uchaguzi mkuu wa mwaka ujao umeanza leo nchini Zimbabwe.
Hii ni mara ya kwanza tangu nchi hiyo kupata uhuru mwaka 1980 ambapo zoezi la kuandikishia wapiga kura litafanyika nje ya Ofisi ya Msajili Mkuu baada ya kupitishwa kwa katiba mpya ambayo imehamisha jukumu hilo kwa Tume ya Uchaguzi ya Zimbabwe.
Tume hiyo imesema inalenga kuandikisha wapiga kura milioni 7 kwa uchaguzi wa mwaka ujao wa urais, wabunge, na serikali za mitaa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |