Mnadhimu mkuu wa jeshi la Uturuki amesema, nchi hiyo imeanza zoezi la kijeshi karibu na mpaka na Iraq.
Zoezi hilo linafanyika wiki moja kabla ya serikali ya eneo la Kurd la Iraq kupiga kura ya maoni kuhusu kujitenga utakaofanyika Septemba 25, jambo linalopingwa vikali na serikali ya Uturuki.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, zoezi hilo limeanza katika maeneo ya Silopi na Habur yaliyoko kusini mashariki mwa Sanliurfa. Pia taarifa hiyo imesema, zoezi hilo ni sehemu ya operesheni za kupambana na ugaidi zinazofanywa na nchi hiyo katika eneo la mpaka.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |