Tume ya uchaguzi ya Russia imetangaza kuwa uchaguzi mkuu wa nchi hiyo utafanyika Machi 18 mwaka kesho, ambapo rais Viladimir Putin anatarajiwa kugombea urais kwenye uchaguzi huo. Bw. Putin mwenye umri wa miaka 64 alichaguliwa kuwa rais wa Russia mwaka 2000, na kushinda muhula wake wa pili kwenye uchaguzi wa mwaka 2004. Mwezi Machi mwaka 2012, Bw. Putin alichaguliwa tena kuwa rais wa Russia kwa muhula wa tatu baada ya baraza la chini la bunge la Russia kupitisha marekebisho ya katiba yanayorefusha kipindi cha urais kutoka miaka 4 hadi 6.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |