Mlipuko wa kujitoa mhanga ulitokea jana katika jimbo la Borno kaskazini mashariki mwa Nigeria na kusababisha vifo vya watu 15.
Ofisa mmoja wa usalama amesema mshambuliaji alijilipua karibu na umati wa watu katika eneo hilo.
Timu ya waokoaji imepelekwa kwenye eneo la mlipuko ili kuwaokoa wahanga wa shambulizi hilo.
Kundi la kigaidi la Boko Haram linashukiwa kuhusika na mlipuko huo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |