Maduka makuu ya Naivas na Carrefour yanawania kuchukua nafasi ya duka lililofungwa la Nakumatt Thika Road Mall (TRM).
Nakumatt, ilitoa tangazo Jumatatu kwamba imefunga duka lake hilo la TRM ili kufanya hesabu za ndani lakini wataalam wa kifedha wanasema kufungwa kwake kunatokana na masaibu ya kifedha yanayokumba maduka hayo.
Mkurugenzi wa jumba la TRM Bashir Dalvi,amesema wanafanya mazungumzo na Nakumatt ili waondoke kwenye nafasi hiyo kwani wamedaiwa esa nyingi za kodi.
Naye mkurugenzi wa oparesheni wa maduka ya Naivas, Willy Kimani amesema wangependa sana kuchukua nafasi hiyo ya TRM.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |