Timu ya JKU imefanikiwa kutwaa taji la ngao ya jamii kuashiria ufunguzi wa msimu mpya wa 2017-2018 wa ligi kuu ya soka visiwani Zanzibar baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Miembeni city katika uwanja wa Amaan jioni ya jana.
Mabao ya JKU yamefungwa na Salum Mussa dakika ya 47 na Nassor Mattar dakika ya 48.
Sasa pazia la ligi kuu ya soka visiwani Zanzibar ndiyo limefunguliwa rasmi na ligi hiyo itaanza rasmi Oktoba 3, 2017.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |