Jumla ya nyota chipukizi 25 wa soka barani Ulaya wametangazwa jana kuwania tuzo ya Europe Golden Boy 2017 ambapo majina, Rashford, Mbappe na Dembele yameonekana kuongoza orodha hiyo.
Tuzo ya Europe Golden Boy hutambua kijana mwenye kipaji zaidi cha soka barani Ulaya chini ya umri wa miaka 21. Kylian Mbappe ambaye alifanya vizuri msimu uliopita akiwa na Monaco msimu huu amehamia PSG na Ousimane Dembele alifanya vizuri msimu uliopita akiwa na Borrusia Dortmund kabla ya kuhamia Barcelona ndio wanatajwa sana huenda wakatwaa tuzo hiyo ambayo itatolewa mwezi Oktoba.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |