Meli ya hospitali ya jeshi la majini la China "Peace Ark" imewasili nchini Sierra Leone, kwa jukumu la kutoa huduma za matibabu bila malipo kwa watu elfu mbili nchini humo kwa muda wa siku nane. Kamanda wa kundi la manowari Bw. Guan Bailin amesema hii ni mara ya kwanza kwa meli hiyo ya Peace Ark kuwasili Afrika magharibi, na operesheni hiyo inalenga kuimarisha ushirikiano kati ya nchi hizo mbili. Makamu wa rais wa Sierra Leone Victor Foh amesema Sierra Leone inaishukuru China kwa michango yake yote tangu uhusiano kati ya nchi mbili uanzishwe mwaka 1971.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |