Mchezaji wa klabu ya Arsenal ya nchini Uingereza, Mesut Ozil amerejea katika mazoezi na timu hiyo baada ya kuwa nje ya uwanja kwa muda akiuguza jeraha lake. Ozil ambaye ni mchezaji wa timu ya taifa ya Ujerumani alikosa mchezo dhidi ya Chelsea katika dimba la Stamford Bridge siku ya Jumapili lakini pia Europa League waliyoshinda 3-0 dhidi ya Cologne.
Ozil pia hakuwa sehemu ya kikosi kilichocheza michuano ya Carabao Cup dhidi ya Doncaster siku ya Jumatano lakini anatarajia kuwafiti hivi karibuni.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |