Mke wa Rais wa Kenya Bibi Margaret Kenyatta ametoa mwito kwa wananchi kuungana na kusameheana wakati Kenya ikiwa kwenye kumbukumbu ya miaka minne tangu shambulizi la kigaidi la Westgate litokee na kusababisha vifo vya watu 67.
Bibi Kenyatta aliyeongoza shughuli ya kumbukumbu hiyo, amesema kumbukumbu ya tukio hilo inaleta maumivu makubwa na masikitiko, lakini pia inawakumbusha wakenya kuungana kwenye mapambano dhidi ya ugaidi.
Amesema shambulizi la Westgate lilivuruga na kubadilisha maisha na ndoto za watu wengi, lakini pia ameonyesha imani yake kwa moyo wa wakenya kuunga mkono shughuli za kuwasaidia watu kama hao na jamii zilizoko hatari.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |