Rais Edgar Lungu wa Zambia ameitaka jumuiya ya kimataifa kutoa msaada kwa Zambia inayopokea idadi kubwa ya watu wa DRC wanaotafuta hifadhi.
Rais Lungu amesema ana wasiwasi kuhusu wimbi kubwa la wakimbizi wanaoingia nchi mwake na wanahitaji msaada ili kuwapokea.
Kuanzia wiki kadhaa zilizopita Zambia imeshuhudia wimbi kubwa la wakimbizi kutoka DRC, na sasa inapokea karibu watu 500 kila siku kutoka nchi hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |