Shirika la afya la duniani la Umoja wa Mataifa (WHO) limehimiza nchi za Afrika kununua dawa zenye bei nafuu na ubora kutoka China na India ili kuokoa maisha zaidi.
Mkurugenzi wa dawa muhimu na idara ya bidhaa za afya bi. Suzanne Hill amesema dawa zenye ubora katika nchi hizo mbili za Asia zimethibitishwa kuwa na ufanisi mkubwa zaidi katika kupambana na magonjwa ya kitropiki. Dawa za kupambana na kama Ukimwi, Malaria pamoja na antibiotic ambazo tayari zinapatikana katika vituo vya afya barani Afrika ambazo zimethibitisha ufanisi wake na kuwapa watu maisha mapya.
WHO imezindua mradi wa kuthibitisha ufanisi wa dawa hizo katika kutibu magonjwa yasiyo ya kuambukizwa (NCDs) hasa kansa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |