Wizara ya ulinzi ya Russia imesema luteni jenerali Valery Asapov ameuawa kwenye shambulizi la mizinga lililofanywa na kundi la Islamic State karibu na mji wa Deir al-Zour, kaskazini mashariki mwa Syria. Taarifa iliyotolewa na wizara hiyo inasema Bw Asapov alikuwa mmoja wa washauri wa kijeshi wa Russia wanaoshirikiana na makamanda wa Syria kwenye operesheni za kuukomboa mji wa Deir al-Zour.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |