Licha ya kusuasua kwenye La Liga, Real Madrid imeonyesha haitaki mchezo na ligi ya mabingwa Ulaya baada ya kuichapa Borussia Dortmund kwa mabao 3-1 ikiwa nyumbani kwao Ujerumani.
Madrid imeshinda kwa mabao 2 ya Cristiano Ronaldo huku nyota wake mwinngine, Gareth Bale akifunga bao la kwanza.
Matokeo ya mechi zingine, Liverpool wamelzimishwa sare ya 1-1 na Spartak, nayo Tottenham ikipata ushindi wa 3-0 dhidi ya Apoel, huku Sevilla wakiifunga Maribor 3-0, nayo Manchester City ikiibuka na ushindi wa 2-0 dhidi ya Shakhtar, Monaco ikipoteza kwa Oporto kwa kufungwa 3-0.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |