Shirikisho la Soka la Rwanda (FERWAFA) limesema mchezo kati ya APR na Rayon Sport ulivunjika jumapili dakika ya 63 kwa sababu ya kukatika umeme uwanjani,utarudiwa kuchezwa leo jumatano.
Mchezo utaanzia dakika ya 63 sekunde ya 42 ambayo ilisimamishiwa mechi hiyo. Katika muda huo Rayon Sport ilikuwa mbele kwa mabao 2-0 dhidi ya APR.
Katika mchezo huo wa leo, APR itaingia uwanjani na wachezaji 10 baada ya mmoja kupewa kadi nyekundu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |