Ujumbe wa sekta ya uchapishaji ya China jana ulifanya maonyesho ya vitabu vinavyoeleza namna ya kuzuia na kutibu magonjwa ya kitropiki, kwenye maonyesho ya kimataifa ya vitabu ya siku tano yaliyofunguliwa huko Nairobi.
Maonyesho hayo yanayoandaliwa na idara ya uchapaji ya Kenya, yanavutia washiriki mbalimbali wa riwaya na vitabu vya mambo halisi.
Mjumbe wa China kwenye maonyesho hayo Bw Chen Yingjie amesema maonyesho hayo yanafahamika sana nchini China, na wamejiandaa vilivyo kwa ajili ya maonyesho hayo.
Bw Chen amesema ushirikiano kwenye mambo ya fasihi kati ya China na Kenya ni moja ya njia za kuimarisha uhusiano kati ya nchi hizi mbili.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |