Kitabu kipya kinachosimulia ujenzi wa serli ya SGR uliofanywa na China nchini Kenya kinatarajiwa kuchapishwa baada ya Shirika la Habari la China Xinhua na kampuni ya Enjoy Culture & Media kusaini makubaliano mjini Nairobi, Kenya.
Kitabu hicho kitakachoitwa "Reli Yangu, Hadithi Yangu" msingi wake ni filamu fupi inayoeleza ujenzi wa reli ya kisasa SGR kati ya Momba na Nairobi nchini Kenya. Filamu hiyo ambayo ilikuwa kwa lugha ya kiingereza, ilitafsiriwa kwa lugha za Kifaransa, Kichina, na hatimaye Kiswahili, imeonyeshwa katika vituo vya televisheni nchini China, Nigeria, na Zambia, pia inapatikana katika mtandao wa internet na mitandao ya kijamii.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |