Kocha Mkuu wa timu za taifa za vijana, Kim Poulsen anatarajiwa kutangaza kikosi cha vijana wenye umri wa chini ya miaka 20 Ngorongoro Heroes huku nyota wa timu hiyo Issa Abdi Makamba akiwa anaendelea vema na matibabu jijini Dar es Salaam. Akizungumzia kuhusu afya ya Makamba ambaye aliumia kidole cha mwisho katika mguu wake wa kushoto, Daktari wa timu hiyo, Shecky Mngazija, amesema mchezaji huyo anaendelea vema na mwezi wa 10 anaweza kuanza mazoezi. Serengeti Boys ni timu ya taifa ya vijana wenye umri wa chini ya miaka 17 ambayo Mei, mwaka huu ilishiriki fainali za AFCON huko Gabon ambako Makamba aliumia kabla ya kuanza kucheza.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |