Watu 15 wamefariki na wengine 50 kujeruhiwa, baadhi yao vibaya, mapema leo katika tukio la kukanyagana lililotokea kwenye daraja la waenda kwa miguu karibu na kituo cha treni mjini Mumbai, India.
Msemaji wa kampuni ya reli Anil Saxena amesema, kazi ya uokoaji inaendelea, na kwamba ni vigumu kwao kutoa idadi kamili ya watu waliofariki, na kwamba taarifa zaidi zitatolewa baadaye.
Amesema serikali ya eneo hilo imeagiza uchunguzi ufanyike ili kujua chanzo cha tukio hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |