Chai ya Rwanda sasa itauzwa chini ya jina mpya Chai ya Taifa ya Rwanda kama njia moja ya kuimarisha imani kwa wateja wao, pamoja na kukuza ushindani wake katika masoko ya ndani na ya kimataifa, Baraza la Taifa la Kilimo (NAEB) imesema.
Issa Nkurunziza, meneja wa muungano wa chai katika Baraza la NAEB,amesema hatua hii inataka kuonyesha thamani ya chai ya Rwanda, na uzuri wake.
Kwa mujibu wa NAEB, chapa hii itawawezesha na kuhamasisha wadau walinaohusika katika mambo ya chai ili kuhifadhi urithi wa nchi hiyo.
NAEB inalenga dola milioni 94.9 kutoka kwa mauzo ya nje ya chai kwa mwaka ifikapo mwaka 2018, kutoka dola milioni 65.7 mwaka 2013.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |