• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Tanzania: Kampuni tatu za nje zatajwa kuchangia kushuka kwa mauzo ya Soko la Hisa

    (GMT+08:00) 2017-10-03 18:21:35

    Kampuni tatu za nje zimechangia kushuka kwa mauzo ya Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) kwa Sh50 bilioni.

    Taarifa ya DSE inazitaja kampuni ambazo hisa zake zimeongoza kushuka kuwa ni Uchumi Supermarket (USL) kwa asilimia 22, Shirika la Ndege la Kenya (KA) asilimia 16 na Acacia kwa asilimia tisa.

    Mauzo ya soko hilo kwa kipindi cha wiki moja yameshuka kutoka Sh53 bilioni mpaka Sh3 bilioni baada ya hisa 800,000 za kampuni za ndani kuuzwa kati ya Septemba 25 hadi Septemba 29.

    Wiki iliyoishia Septemba 22, jumla ya mauzo ilikuwa Sh53 bilioni, lakini wiki iliyoishia Septemba 29 yalikuwa Sh3 bilioni.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako