Kampuni ya kusaga unga nchini Kenya Unga Group, imepata hasara ya shilingi milioni 32 katika kipindi kilichokalimika Juni 2017.
Unga Group imepata harasa hiyo licha ya kuwepo na mahindi ya bei rahisi iliotolewa na serikkali.
Awali mwaka huu kampuni hiyo ilikuwa imetoa ilani ya kupata hasara kufuatia kiangazi na ukosefu wa nafaka.
Inasema mahindi ya bei rahisi yaliotolewa na serikali yalifika mwishoni mwa kipindi chake cha fedha na hivyo yangesaidia sana kuongeza faida.
Serikali ilikuwa inauzia kampuni za kusaga unga mahindi kwa bei ya 2,300 huku bei ya kawaida ikiwa ni shilinghi 4,000 kwa gunia la kilo 90.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |