Wataalamu wa masuala ya fedha na kilimo wa Uganda wamesema kuna uwezekano wa wakulima wastani na wale wa kilimo cha chakula na matumizi ya nyumbani . kupata mikopo kupitia teknolojia ya kisasa.
Hii ni baada ya kuanzishwa kwa mpango wa pesa za wakulima maskini na hazina ya maendeleo ya Umoja wa Mataifa .
Catherine Denis muanzilishi wa mradi huo amesema zaidi ya asilimia 70 ya waganda ,hutegemea ajira ya kilimo hivyo watawafikia wakulima wasiojiweza kifedha kuwapa mtaji wa kilimo cha biashara.
Wadau wa sekta ya benki ,na data za dijitali wamekutana kujadiliana kuhusu swakla hili na kukubaliana kufanya kazi pamoja na kuwainua wakulima.
Wakulima sasa watasajiliwa kupitia kwa vyama vya ushirika kabla ya kupewa mikopo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |