• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Wateja wa benki ya Chase bank ya Kenya waangalia kupoteza asilimia 25 ya akiba zao

    (GMT+08:00) 2017-10-09 19:30:26
    Wateja walikuwa wameweka pesa na Benki ya Chase Bank wanangalia kupoteza asilimia 25 ya fedha zao chini ya muundo mpya ambao umeona taasisi hiyo ikichukuliwa na Benki ya Taifa ya Mauritius (SBM).

    Siku ya Ijumaa, Benki Kuu ya Kenya ilibainisha kwamba SBM itachukua zaidi ya asilimia 75 ya Sh bilioni 76 iliyoshikiliwa katika akaunti zilizozuiwa ndani ya Benki ya Chase.

    Kulingana na Gavana wa, Benki Kuu ya Kenya (CBK) Patrick Njoroge, wateja walikuwa wameweka fedha na benki hiyo watapata sh bilioni 57 kuanzia Januari 1, 2018, lakini katika awamu tatu ambazo zitaenda hadi 2021.

    Njoroge hakutoa mwelekeo wowote kwa Sh bilioni 19 iliyobaki katika Benki ya Chase Bank , jambo ambalo limewaacha wateja wa Benki hiyo na hofu ya watapoteza akiba zao.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako