Kwa mara ya kwanza Iceland wamefuzu kombe la dunia huku wakiongoza kundi lao la I baada ya jana kuibuka kidedea kwa goli 2-0 dhidi ya Kosovo, magoli yamefungwa na Sirgudsson na J Gudmundsonn.
Kwingineko, Antonio Candreva amefunga bao moja na kuisaidia timu yake ya Italia kuifunga Albania huku Hispania ambao wamekwishajikatia tiketi ya kucheza michuano hiyo wakiichapa Israel goli 1-0. Katika kundi D timu ya taifa ya Wales wakiwa nyumbani walikubali kipigo cha goli moja kwa nunge kutoka Ireland, huku Serbia nao wakiwa nyumbani wakaichapa Georgia 1-0.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |