Serikali ya Uganda sasa itakagua shughuli zote za upakiaji wa maji ya kunywa kwenye chupa ili kuhakikisha usalama wa bidhaa hiyo kwa wananchi.
Baraza la mawaziri tayari limepitisha sera ya kuthibiti sekta ya biashara ya maji kote nchini humo.
Wakfu wa wenye biashara nchini humo umesema hatua hiyo ya serikali itasaidia kuongeza ubora na usalama wa maji.
Taakwimu za wizara ya viwanda nchini humo inaonyesha kwamba sektaya upakiaji maji inaajiri kwa jumla karibu watu 15,000 huku ikichangia shilingi bilioni 150 kwa pato la kitaifa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |