Serikali ya Rwanda iko kwenye harakati za kupiga marufuku uagiziaji wa mbegu hasa za Soya na ngano.
Mkurungezi wa halmashauri ya kilimo nchini humo Mark Cyubahiro Bagabe amesema serikali inawekeza kwenye uzalishaji wa ndani ya nchi wa mbegu ili kuwa na suluhu la muda mrefu.
Alisema serikali inalenga kujitegemea na mbegu ifikapo mwaka 2021 za mahindi, ngano na soya.
Kwa sasa Rwanda inaagizia mbegu za mahindi kutoka Zambia, ngano kutoka Kenya na soya kutoka Zimbabwe.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |