Rais wa shirikisho la soka nchini Tanzania (TFF) Wallace Karia pamoja na kaimu katibu mkuu, Kidao Wilfred wametembelea makao makuu ya shirikisho la soka barani Afrika CAF na kukutana na Rais wa shirikisho hilo Bw. Ahmad Ahmad.
Mara baada ya kuwasili na kupokelewa na mwenyeji wao, walifanya kikao kilichojadili maendeleo ya soka nchini Tanzania.
Rais wa CAF ameahidi kuisaidia TFF katika mipango ya maendeleo ya soka ili kuongeza umoja kwasababu soka siku zote hujenga umoja na mshikamano.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |