• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Sudan Kusini yakubali kufanyika kwa majadiliano kwa pamoja kuhusu makubaliano ya amani

    (GMT+08:00) 2017-10-12 09:50:58

    Ofisa mwandamizi wa Sudan Kusini amesema vyama mbalimbali vinavyounda serikali ya mpito ya umoja wa kitaifa, vimekubali kufanyika kwa majadiliano ya pamoja kuhusu kufufua makubaliano ya amani yaliyoandaliwa na Shirika la maendeleo la kiserikali ya nchi za Afrika Mashariki IGAD.

    Waziri wa habari wa nchi hiyo Bw. Michael Makuei amesema, wamepokea barua kutoka kwa IGAD na kukubaliana kufanya majadiliano kwa pamoja, badala ya kufanya mazungumzo na chama kimoja kimoja.

    Barua hiyo imekuja baada ya kiongozi wa chama cha SPLM-wapizani Bw. Dhieu Mathok kutoa wito kuhimiza kufanyika majadiliano ya pamoja.

    Bw. Mathok amesisitiza kuwa serikali ya mpito ya umoja ya kitaifa ni chombo muhimu cha kutekeleza makubaliano ya amani.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako