Mgomo wa daladala jijini Tanga nchini Tanzania umeingia siku ya pili leo Jumanne, Oktoba 17 huku waendesha bodaboda, bajaji na baiskeli wakitumia fursa hiyo kutoa huduma na kujiongezea kipato.
Mgomo huo pia umesababisha watu wengi kutembea kwa miguu kwenda maeneo mbalimbali jijini Tanga.
Baadhi ya abiria wamesema wamelazimika kukodi bodaboda baada ya kukosa huduma ya daladala.
Amesema mgomo huo wa daladala umesababisha abiria kukodi bajaji na kulipa nauli kwa kuchangia.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |