• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Tanzania:TBL yaongoza mauzo katika Soko la Hisa Dar es Salaam

    (GMT+08:00) 2017-10-17 19:19:02

    Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) imeongoza mauzo katika Soko la Hisa Dar es Salaam (DSE) na kuwapa faida ya kati ya asilimia 2.3 mpaka 7.7 waliofanya miamala hiyo kwa wiki iliyoisha Oktoba 13.

    Licha ya kupanda kwa hisa za TBL, mauzo ya DSE yamepanda kutoka Sh1.5 bilioni wiki iliyoishia Oktoba 6 hadi Sh30 bilioni ilipofika Oktoba 13 na hisa zilizouzwa zikiongezeka kutoka 600,000 hadi milioni 2.5.

    TBL iliongoza mauzo hayo kwa asilimia 99.6 ikifuatiwa na Benki ya CRDB kwa asilimia 0.2 na Vodacom asilimia 0.1.

    Meneja mkuu wa kampuni ya Orbit Securities, Simon Juventus alisema TBL inakimbiliwa kwa sababu imetangaza gawio la Sh470 kwa kila hisa kwenye awamu ya pili baada ya kutangaza Sh100 katika awamu ya kwanza.

    Alisema kampuni inayofanya vizuri sokoni huvuta macho ya wawekezaji wengi hasa kunapokuwa na mambo yanayotarajiwa kama ilivyo kwa gawio.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako