Serikali ya Norway imetoa shilingi bilioni 2 kwa wanawake wakimbizi kutoka Sudan Kusini waliopo nchini Uganda.
Fedha hizi zitatumika kuwawezesha wanawake hao kwa mitaji ya biashara pamoja na kupewa mafunzo maalum.
Susan Eckey balozi wa Norway nchini Uganda ameshinikiza kwamba fedha hizo zitawapa fursa wakimbizi hao kufanya biashara na kujitegemea.
Shirika la umoja wa mataifa (UN)aidha limeanzisha mpango maalum wa miaka mitatu wa kuwawezesha wanwake katika maendeleo ya uchumi.
Wanawake hao vile vile watafunzwa lugha ya Kiingereza na kuunganishwa na masoko ya bidhaa zao.
Zaidi ya wakimbizi 3lfu 6 watafaidika .
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |