Halmashauri ya ushuru nchini Uganda imeanzisha tena upya kampeini ya kuhamasisha watu kulipa ushuru.
Ian Rumanyika kupitia kwa mahojiano na vyombo vya habari amesema watu wengi hawalipi ushuru kutokana na kukosa ufahamu.
Oparesheni ya kuhamaisha umuhimu wa kulipa ushhuru ilianzishwa mwezi uliopita na sasa maafisa wa ushuru wataanza kupiga doria ya kuwatia mbaroni wahalifu wanaokwepa ushuru kwa kukusudia.
Uganda inajizatiti kuongeza mapato ya serikali kupitia kwa ukusanyaji wa ushuru.
Aidha mbinu za kisasa za dijitali za kulipa ushuru zimeanzishwa na zinatumika katika vituo 75 kote Uganda.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |