Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya amefungua kesi katika mahakama kuu ya Kenya, akiitaka mahakama hiyo iwape adhabu ya kifungo kwenye jela la kiraia kwa muda wa miezi sita kwa kuipuuza mahakama.
Muungano wa Jubilee unaoongozwa na Rais Kenyatta umesema maandamano makubwa yanayoitishwa na muungano wa upinzani NASA katika baadhi ya maeneo ya Kenya, ni ukiukaji wa amri ya mahakama, ambayo iliamuru uchaguzi mpya wa Rais ufanyike ndani ya siku 60. NASA wameitisha maandamano kwa muda wa wiki tatu kutaka mageuzi kwenye tume ya uchaguzi na kuondolewa kwa baadhi ya wafanyakazi wake kabla ya uchaguzi mkuu.
Maandamano hayo yamesababisha vifo katika eneo la magharibi la Kenya, lakini yalisimamishwa kwa muda ili kuomboleza vifo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |