Wizara ya afya ya Uganda imethibitisha kuwa mlipuko wa homa ya Marburg umetokea kwenye eneo la Kween, mashariki mwa nchi hiyo. Waziri wa afya wa Uganda Bibi Jane Aceng amesema timu ya madaktari inayoongozwa na kaimu mkurugenzi wa huduma za afya Bw Anthony Mbonye imepelekwa kwenye eneo hilo kudhibiti mlipuko wa homa hiyo, na kwamba wizara yake imeanzisha vituo vya karantini kuwashughulikia watu wote wanaodhaniwa kuambukizwa homa hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |