Jeshi la serikali ya Iraq limethibitisha kuwa, jana limepambana na wapiganaji katika mpaka kati ya mkoa wa Kirkuk na eneo la Wakurd.
Taarifa iliyotolewa na jeshi hilo inasema, jeshi hilo lilipoingia mji wa Altun Kupri mkoani Kirkuk ambao uko karibu na eneo la Wakurd, lilipambana na wapiganaji wa kundi la Peshmerga lililomilikiwa na serikali ya Wakurd. Wapiganaji wa Kikurd walirushia makombora jeshi la serikali, na kusababisha vifo na majeruhi ya watu na hasara ya mali.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |