Ligi kuu ya Uingereza imeendelea wikiendi iliyoisha, Manchester City ikiifunga Burnley goli 3-0. Mabao ya Man City yaliwekwa kimiani na Sergio Aguero, Nicolas Ota,endi na Leroy Sane.
Manchester United chini ya kocha wake mwenye maneno mengi Jose Mourinho imejikuta ikiambulia kichapo cha 2-1 dhidi ya Huddersfield.
Chelsea imeibuka na ushindi wa goli 4-2 dhidi ya Watford, mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa Stamford Bridge. Arsenal imeona mwezi baada ya kuibandika Everton goli 5-2, huku Liverpool ikichezea kichapo cha 4-1 toka kwa Tottenham Hotspur.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |