Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Bw. Rex Tillerson amesema sasa umefika wakati wa kutatua mgogoro wa nchi za ghuba.
Katika mkutano na wanahabari uliofanywa kwa pamoja na Bw. Tillerson na wenzake wa Qatar Bw. Sheikh Mohammed Bin Abdulrahman Bw. Tillerson amesema rais Donald Trump wa Marekani amewasiliana na viongozi wa nchi husika, na kusisitiza kuwa sasa umefika wakati wa kutatua mgogoro huo.
Naye Bw. Mohammed amesema Qatar inashikilia kufanya mazungumzo kwenye msingi wa kutodhuru sera za nchi na sheria za kimataifa.
Bw. Tillerson alianza ziara yake nchini Qatar baada ya kumaliza ziara yake nchini Saudi Arabia.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |