Mwanariadha Joycelline Jepkosgeai amedhihirisha kuwa malkia wa mbio za kilomita 21 baada ya kuvunja rekodi yake ya dunia na kutwaa ubingwa wa Valencia half marathon nchini Uhispania mwishoni mwa wiki.
Jepkosgei alitumia saa 1:04:51 na kuweka rekodi ya 6 kwa mwaka huu kwa kushinda rekodi nyingine za kilomita 10, kimolita 15 na kilomita 20.
Kwa upande wa wanaume, taji la Valencia half marathon limenyakuliwa na Abraham Cheroben raia wa Bahrain baada ya kutumia dakika 59:11
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |