Mkurungezi wa maduka hayo Atul Shah hajaelezea kuhusu kufungwa kwa maduka hayo lakini amesema atatoa taarifa baadaye.
Nakumatt imekuwa ikifunga matawi yake ambayo hayana mauzo mazuri nchini Kenya, Uganda na Tanzania.
Wiki jana tawi lake moja katika eneo la Mlimani City mjini Dar es Salaam lilifungwa kutokana na deni kubwa la kodi ya nyumba.
Baadhi ya matawi mengine yaliofungwa nchini Kenya ni Lunga Lunga mjini Mombasa na Nairobi matawi ya Thika Road Mall, Next Gen na Westgate.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |