• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Tanzania-Huduma za kibenki ziongezwe vijijini,asema makamu wa rais Samia Suluhu

    (GMT+08:00) 2017-10-25 18:15:46
    Makamu wa Rais wa Tanzania Samia Suluhu amewahimiza wadau wa benki kuongeza juhudi za kuwafikia wanawake wa ngazi za chini.

    Samia alisema pamoja jitihada zinazofanywa na wadau wa benki mbalimbali kufanikisha mpango wa kuondoa maskini,bado wanawake wa ngazi ya chini hawajafikiwa kikamilifu.

    Bi Suluhu aliyasema hayo jana wakati akifungua mkutano wa dunia wa wanawake na huduma za kibenki wenye kaulimbiu ya "Kuwapa fursa za kibenki wanawake".

    Mkutano huo wa siku mbili ambao unafanyika jijini Dar es Salaam umevutia washiriki zaidi ya 300 kutoka nchi 40 duniani na ni wa kwanza kufanyika Afrika.

    Aidha Samia aliitaka Benki ya Wanawake Tanzania (TWB) ambayo ilianzishwa mahsusi kwa ajili ya kuwawezesha wanawake kujikwamua na umaskini ,iongeze kasi ya kuwafikia wanawake ,hususan wa vijijini kwa kuongeza matawi karibu na wananchi.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako