Jeshi la Libya limefanikiwa kuvunja jaribio la kusafirisha silaha kwenda nchi jirani ya Sudan. Kamanda wa batalioni ya Subul Assalam Bw. Abdarrahman Al-Kilani amesema batalioni yake imezuia jaribio hilo la kusafirisha silaha na risasi kwenda Sudan, baada ya wakazi wa mji wa Kufra kulalamika kuwa wafanyabiashara ya silaha wamefikia makubaliano na kundi moja haramu la Sudan kununua silaha na risasi, na kikosi chake kiliwakamata wahusika na silaha hizo kilomita 300 kusini ya mji huo. Amesema uchunguzi kuhusu tukio hilo bado unaendelea.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |