Serikali ya jimbo la wakurdi nchini Iraq imependekeza kusitisha utekelezaji wa matokeo ya kura za maoni, ili kutandika njia kwa ajili ya mazungumzo na serikali kuu. Taarifa iliyotolewa na serikali hiyo imesisitiza kuwa jimbo hilo halina nia ya kupambana na serikali kuu, na itasitisha mara moja operesheni zote za kijeshi katika jimbo hilo. Serikali kuu ya Iraq bado haijatoa maoni kuhusu taarifa hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |