Watu wasiopungua 10 wameuawa na wengine zaidi ya 16 wamejeruhiwa baada ya msafara wa magari ya tume ya Umoja wa Afrika nchini Somalia AMISOM kukanyaga bomu la kutegwa ardhini jana kusini ya Mogadishu.
Ofisa wa usalama amesema tukio hilo limetokea katika eneo kati ya Arbiska na Lafole karibu na wilaya ya Afgoye, kilomita 30 kusini ya Mogadishu.
Msemaji wa vikosi vya AMISOM Bw Wilson Rono amethibitisha kwamba wahanga hao wameuawa katika mapambano kati ya vikosi vya Umoja wa Afrika na waasi wa Kundi la Al-Shabaab. Amesema askari mmoja wa AMISOM ameuawa na mwingine amejeruhiwa.
Kundi la Al-Shabaab halijasema lolote kuhusu tukio hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |