Jeshi la serikali ya Syria limesema linakaribia eneo la al-Bukamal ambalo ni ngome muhimu ya mwisho ya kundi hilo karibu na mpaka wa Iraq.
Jeshi la Syria linapigania kudhibiti tena eneo la visima vya mafuta ili kufika al-Bukamal, siku kadhaa baada ya jeshi hilo kuukomboa mji wa al-Mayadeen, ambao ulichukuliwa kama ni mji mkuu wa IS katika jimbo la Deir al-Zour.
Al-Bukamal ni muhimu kwa kundi la IS kutokana na ukaribu wake na maeneo yanadhibitiwa na kundi hilo katika upande wa Iraq.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |