Rais Vladmir Putin wa Russia ametoa pongezi kwa rais Xi Jinping wa China kuchaguliwa tena kuwa katibu mkuu wa Chama cha Kikomunisti cha China. Rais Putin amesema matokeo ya uchaguzi yamethibitisha heshima ya kisiasa ya rais Xi Jinping, na kuonesha kuwa dira aliyoitoa kuhusu kuharakisha maendeleo ya uchumi na jamii ya China na kuimarisha hadhi ya kimataifa ya China imekubaliwa na watu wengi.
Rais Putin amesema anaamini kwamba uamuzi uliotolewa kwenye mkutano mkuu wa 19 wa Chama cha Kikomunisti cha China utasaidia kuimarisha uhusiano wa wenzi wa kimkakati kati ya China na Russia, na anatarajia kuzidi kuendeleza ushirikiano kati ya nchi hizo mbili, na kusukuma mbele ushirikiano wa kiujenzi katika mambo ya kikanda na kimataifa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |