• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Rwanda:Bodi ya kilimo ya Rwanda yalenga kuimarisha kahawa

    (GMT+08:00) 2017-10-26 20:10:56
    Siku chache baada ya kahawa ya Rwanda kuorodheshwa miongoni mwa kahawa bora Duniani ,halmashauri ya kitaifa ya mauzo ya nje imetangaza kuanzisha mradi mpya wa kuhakikisha inakuwa kahawa ya kwanza duniani.

    Rwanda imezishinda nchi nane za kuzalisha na kuuza kahawa zikiwemo Brazil,Colombia,Costa Rica,Ethiopia India na nyinginezo.

    Jean Paul Ndamwemera meneja wa Lisa Coffee ya Rwanda amesema ushindi huo utafungua masoko mapya na kuwavutia wateja wapya.

    Muungano wa wauzaji wa kahawa Rwanda umepanga kushirikiana na wakulima ili kuongeza uzalishaji na uboreshaji wa kahawa.

    Rwanda ilipata dola milioni 58.5 kutoka kwa uuzaji kahawa mwaka jana.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako