Aliyekuwa jaji mkuu wa Tanzania Bw Mohamed Othman aliyepewa jukumu la kuchunguza ajali ya kuanguka kwa ndege iliyosababisha kifo cha aliyekuwa katibu mkuu wa Umoja wa mataifa Bw. Dag Hammarskjold, ametoa ripoti ya uchunguzi ikisema ajali hiyo huenda ilitokana na shambulizi na tishio la nje. Ripoti pia imeondoa uwekezano wa kutokea kwa hitilafu za kiufundi kwenye ndege hiyo, lakini haijafuta uwezekano wa makosa ya kibinadamu yaliyosababisha ajali hiyo. Ripoti hiyo imewasilishwa kwa mwenyekiti wa Baraza kuu la Umoja wa mataifa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |